Friday, 8 October 2010

Video Production HVR-Z5P SONY HDV

saratani ya ngozi kwa albino ni janga la taifa

http://www.mwananchi.co.tz/makala/-/5357-saada-saratani-inakula-uso-wangu

Na Florence Majani.gazeti Mwananchi Oct 7, 2010

MSISIMKO wa ajabu lazima ukukumbe pale utakapokutana naye akiwa na kidonda kilichosababisha shimo katika mwamba wa pua yake.  Huku juu ya shavu lake la kulia kuna kovu la kidonda nacho kikiwa kimetengeneza shimo na kuufanya uso wake uwe wa kustaajabisha.
Saada Rashid amezaliwa  Ifakara, Morogoro, miaka 30 iliyopita akiwa ni binti  pekee kwa wazazi wake. Amezaliwa na  ulemavu wa ngozi huku akitoka katika familia yenye kipato duni, hivyo  maisha yake kuwa ya kubahatisha kila kunapokucha.
Anasema, kwa bahati mbaya mama yake alifariki mwaka 2005, na kwa sababu asingeweza kuishi kwa mama wa kambo ilimbidi akaishi kwa shangazi yake na huko hali haikuwa shwari.

“Shangazi yangu naye hakuwa na maisha mazuri, tulikuwa na maisha ya tabu, baya zaidi mjomba wangu alikuwa hanitaki na alipenda   kulalamika sana. Maneno yake ya chinichini yalizidi baada ya mimi kupata ujauzito. Mjomba alidiriki kumtamkia shangazi kuwa hanitaki kama nisingeondoka basi angemfukuza hata na shangazi,”anasema Saada
Kwa bahati mbaya Saada alipachikwa ujauzito huo na mume wa mtu, ambaye mbali na kuwa na watoto, pia hana shughuli yoyote ya kumuingizia kipato.

Maisha ya Saada yalikuwa hatarini na hakuwa na muelekeo baada ya shangazi yake kuitii amri ya mjomba wake na kumfukuza.
“Nilipojifungua tu ndipo nilipofukuzwa rasmi nyumbani kwa shangazi yangu, nikaamua kujitafutia mahali pa kuishi, sikuwa na ndugu yoyote, nikachukua uamuzi wa kwenda katika nyumba ya masista, kituo cha masista cha kulea watu wenye ukoma. Nikaomba wanipe msaada mimi na mwanangu kwa bahati nzuri nilimkuta sista mmoja, Maria Paulo huyo alinionea huruma na akanisaidia nikaanza rasmi kuishi katika kituo hicho,” anasema  Saada.

Hakupenda kuishi katika kituo kile, alitamani ajitegemee na  amlee mtoto wake wa kike aliyempa jina la Swaiba. Akamuomba sista Maria ampe fedha za kujikimu akaanze maisha kijijini kwao Ifakara.
“Nikamuomba sista Maria anipe msaada ili nikatafute kiwanja nianze maisha ya kujitegemea, akaniambia anao uwezo wa kunipa shilingi laki nne tu na akasema hana fedha zaidi ya hizo. Nikasaidiwa kupata kiasi hicho cha fedha  nikaenda kijijini kwetu nikanunua kiwanja kwa shilingi 70,000, na kisha nikajenga nyumba ya matofali ya kuchoma, nikawa nalima napata chakula kidogo,”anasema.

Baada ya muda akaanza kuona kidonda kidogo katika paji lake la uso, akaenda hospitali  ya Ifakara akatibiwa kwa kutiwa dawa na  kufungwa lakini kidonda kile hakikupona kabisa na ndipo alipopewa barua ya kwenda hospitali ya taifa ya  Muhimbili.
“Pale Muhimbili nikafanyiwa vipimo  madaktari wakasema haikuwa kansa ni vidonda vya kawaida nikapewa dawa za kunywa na kupaka nikarudi Ifakara lakini kidonda kile hakikupata nafuu yoyote nikaenda  tena Muhimbili.
Safari hii nikakwanguliwa nyama ya paji la uso pale kwenye kidonda halafu wakanikata nyama katika paja langu la kulia na kuziba shimo la kwenye  uso,”anaelezea Saada.
Hata hivyo amani ya Saada haikudumu kwa muda mrefu kwani   October 2008, kikaanza kidonda kipya, safari hii kikiwa juu kidogo ya sikio. Hata hivyo hakuweza kufanya lolote kwa sababu hakuwa na fedha hata za kula yeye na mtoto wake na kipindi hicho alikuwa amebeba  ujauzito wa pili.

“Nikashindwa kwenda hospitali sikuwa na fedha kabisa, nikaamua kwenda kwa shangazi yangu kumuomba msaada kwani kidonda kilikuwa kinaniuma na sikuwa nikilala usiku isitoshe nilikuwa nina ujauzito wa mtoto huyu. Watoto wa shangazi wakachanga shilingi elfu tano tano kila mmoja wakanipa niende hospitali,”anaeleza.
Kile alichokitegemea hospitali ya Ifakara sicho alichokipata, kwani baada ya madaktari kumpima wakashauri akatwe sehemu ya nyama yake ili ikapimwe Ulaya na hapo alitakiwa atoe shilingi 30,000.

“Sikuwa na fedha hizo ndipo wakaniambia niende Ocean Road, wakaniambia nisubiri barua, niliisubiri kwa miezi mitatu hadi Desemba 2009 ndipo nilipopewa na   kuipeleka Ocean Road, sikuwa na nauli.  Nikaamua kumtafuta yule sista Maria aliyenisaidia kipindi kile nikaenda katika kituo alichokuwa akikaa kwa bahati mbaya nikaambiwa mtu huyo alikwisharudi Ulaya. Nilikosa nguvu nikakata tamaa, nikajikaza na kuwaelezea matatizo yangu  nikawaambia sipajui Dar es Salaam wala sina ndugu  wakanipa 20,000,”anasema Saada.

Nauli ya kutoka Ifakara kwenda Dar es Salaam, ilikuwa ni shilingi 20,000 hivyo mkononi mwake alikuwa na kiasi hicho tu bila akiba ya matumizi mengine akiwa na mtoto mdogo wa miezi mitano mgongoni mwake.
“Ikanibidi nitafute mtu wa kumuachia mtoto yaani Swahiba nikamuacha kwa shangazi yangu. Kwa bahati nzuri nikiwa katika gari nikakutana na msamaria mwema, mama Shukuru ambaye alinipa msaada mkubwa. Nilipofika hapa Dar   es Salaam nikafikia nyumbani kwake Yombo. Asubuhi siku iliyofuata akanileta hapa Ocean Road,”anasimulia Saada.

Alipofika Ocean Road madaktari wa pale walimwambia aende Muhimbili akachukue  kwanza vipimo  ili wavifanyie kazi. Hatua za uchukuaji wa vipimo hivyo haukuwa wa siku moja na ilimbidi apewe kitanda  lakini hilo halikuwezekana.
“Muhimbili walikataa mimi kulazwa nikiwa na mtoto wa miezi mitano, ikanibidi nikae kwa mama Shukuru huku nikiendelea kufanya  vipimo nikawa nasaidiwa nauli na jirani mwingine kwa sababu hata mwenyeji wangu hakuwa na uwezo wa kunipa nauli ya kila siku,” anasema Saada.

Anasema, machi 23 mwaka huu akafanikiwa kupelekwa Ocean Road akagundulika kuwa saratani inamla sehemu za usoni na kwenye ubongo. Ndipo madaktari wakaamua aanzishiwe tiba ya mionzi.
“Nikaanza na tiba ya mionzi, nikapigwa mionzi 10 mara ya kwanza na mara ya pili nikapigwa mionzi saba nikaruhusiwa na  kuambiwa nirudi tena  Septemba 15,”anaeleza.

Kabla ya tarehe ya kurudi kiliniki kikaanza kidonda cha puani, kila alipoenda kukitibu hospitali hakikupona, ndipo alipoamua kutafuta nauli na alipopata alipanda treni na kuja Dar es Salaam.
“Nilifikia tena kwa mama Shukuru, nikapewa kitanda hapa Ocean Road nikaanza matibabu nikakatwa tena nyama hapa puani na nikaendelea na tiba ya mionzi,”anasema.

Pamoja na kuugulia maumivu makali yasababishwayo na saratani  inayomla katika uso wake, inambidi Saada akae na mtoto wake  mdogo mwenye mwaka mmoja hospitalini hapo.  Uso wake unaendelea kumegwa siku hadi siku kwa sababu kansa hiyo ipo mwilini mwake, hana msaada wa kifedha kwake na mtoto wake.

Kwa huzuni huku machozi  yakimtoka Saada anasema, “Sikupenda kuwa hivi, napata mateso makali sana. Natamani kupona, natamani kufanya kazi lakini sijasoma nimekomea darasa la nne hata hivyo naweza kufanya kitu cha kuniingizia fedha kwa kukodi shamba na kutafuta  vibarua watakaolima, kwa sababu nimeambiwa nisikae juani”.

Leo ni Saada na kesho ni wewe, mzazi wako au  ndugu yako haya humkuta kila mtu mwenye pumzi bila kupanga wala kupenda. Maisha yake ni ya taabu anahitaji msaada wako kwani hakupenda kuwa mlemavu na wala hakuombea saratani hii imtafune usoni.
Kwa yeyote ambaye anapenda kumsaidia anaweza kuwasiliana na mwandishi wa makala haya 0715773366

Thursday, 7 October 2010

TAMKO LA FEMACT KUHUSU KAULI YA JWTZ JUU YA UCHAGUZI

C/O TANZANIA GENDER NETWORKING PROGRAMME, MABIBO ROAD,
P O BOX 8921, DAR ES SALAAM, TEL. +255 22 2443205;2443450;2443286
Mobile 255 754 784 050 Fax. 2443244, Email
info@tgnp.org, web TGNP

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA VISIINGILIE UCHAGUZI MKUU; KUVURUGA AMANI

1. Oktoba 1, 2010, Vyombo vya Ulinzi na Usalama; Makao Makuu ya Jeshi
la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Makao Makuu ya Jeshi ka Polisi
vilitoa tamko, kupitia Luteni Jenerali Abdulhaman Shimbo, Mnadhimu
Mkuu wa JWTZ, juu ya ulinzi na usalama kuhusu amani wakati wa kampeni
na uchaguzi. Kesho yake, yaani Oktoba 2, vyombo vya habari nchini
vilikariri tamko hilo, na hivyo kusambaza ujumbe na maudhui yake kwa
wananchi na umma kwa ujumla, kama ilivyokusudiwa.

2. Katika ujumla wake, Tamko la Vyombo vya Ulinzi na Usalama
linasisitiza umuhimu wa wadau wa uchaguzi kulinda amani na usalama,
ambazo ni tunu za Taifa la Tanzania, hususan katika kipindi hiki cha
kampeni kuelekea Uchaguzi Mkuu 2010. Tamko linawakumbusha wadau wa
uchaguzi; wananchi, asasi za kiraia, mashirika ya dini na vyama vya
siasa, umuhimu wa kutunza na kuenzi amani sawia na kushirikiana na
vyombo vya usalama kulinda amani. Aidha wadau wanakumbushwa wajibu wa
majeshi; JWTZ na polisi kuhakikisha kuwa nchi inaendelea kuwa katika
hali ya amani na usalama. Hili ni jambo jema kwa faida na ustawi wa
taifa letu ambalo wengi wa wananchi wake bado ni maskini sana.

3. Hata hivyo, licha ya Tamko kuwakumbusha Watanzania umuhimu wa
kuenzi na kulinda amani na usalama wa taifa lao, sisi mashirika
yanayotetea Usawa wa Jinsia, Haki za Binadamu na Maendeleo na Ukombozi
wa Wanawake Kimapinduzi (FemAct) tumeshitushwa, hatukubaliani na
tunalaani kwa jinsi na namna (mtindo) tamko la vyombo vya ulinzi na
usalama lilivyotolewa, uhalali wa wahusika kutoa tamko hilo, kipindi
lilipotolewa tamko hilo, mantiki yake, mwelekeo wa maudhui yake na
chombo kilichotoa tamko husika kwa sababu zifuatazo:

i). Tamko la Vyombo vya Ulinzi na Usalama linakiuka, na ni kinyume cha
Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya 1977. Ibara 138 haibainishi kuwa
Majeshi ya Ulinzi na Usalama yatajihusisha moja kwa moja na masuala ya
Uchaguzi wala kubainisha kuwa Amiri Jeshi Mkuu, yaani Rais wa Jamhuri,
anaweza kutoa amri kwa majeshi ya Ulinzi na Usalama kuingilia shughuli
za Uchaguzi Mkuu, au chaguzi nyinginezo. Aidha ibara ya 74 ya Katiba
ya Jamhuri ya Muungano ya 1977, haitaji wala kutambua Majeshi ya
Ulinzi na Usalama kama sehemu ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi. Kitendo
cha Majeshi ya Ulinzi na Usalama kutoa tamko kupitia vyombo vya habari
ni dhahiri kinalenga kutoa vitisho, kuchochea, kuingilia mchakato, na
bila shaka kuvuruga Uchaguzi Mkuu unaokusudiwa kufanyika Oktoba 31. Na
kama hivyo ndivyo, WanaFemAct tunalazimika kuamini kuwa tamko la
vyombo vya Ulinzi na Usalama limeficha na kusheheneza malengo ya
maslahi binafsi, siyo maslahi ya nchi kama umma unavyoaminishwa.

ii). Hadi sasa, zaidi ya 'vijembe' vya hapa na pale baina ya wanasiasa
na vyama vya siasa vinavyoshindana na kujinadi kwa wananchi ili kupata
ridhaa ya kuongoza dola ya Tanzania, hakuna wala hakujatokea tishio
lolote la kuvurugika kwa amani. Vyama vya Siasa vimekuwa vikiendelea
kutangaza mipango ya sera zao, vijijini na mijini, kupitia mikutano ya
kampeni; wananchi wamekuwa wakijitokeza kwa wingi kuhudhuria mikutano
ya kampeni, kusikiliza na kuchambua ahadi mbalimbali zinazotolewa na
wanasiasa na vyama vyao; vyombo vya habari vimekuwa vikiripoti taarifa
mbalimbali kuhusiana na mambo yanayojiri kwenye mikutano ya kampeni,
na hata kampeni za nyumba kwa nyumba; asasi za kiraia, kwa
kushirikiana na Tume ya Taifa ya Uchaguzi, zimekuwa zikiendelea kutoa
elimu ya mpiga kura kwa makundi mabalimbali ya wapiga kura watarajiwa;
Msajili wa Vyama Vya siasa amekuwa akiendelea kufuatilia utekelezaji
wa Maadili ya Vyama vya Siasa Wakati wa Uchaguzi Mkuu 2010 na Sheria
ya Gharama za Uchaguzi; na Tume ya Taifa ya Uchaguzi imekuwa
ikiendelea kuratibu kampeni, kusimamia manunuzi ya vifaa tayari kwa
kusambazwa katika vituo 52 000 vya kupigia kura nchini kote,
kuthibitisha usahihi wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura, na kuratibu
wadau wengine wa uchaguzi, kwa mfano, waangalizi wa ndani na nje wa
uchaguzi. Hayo yote yakiwa yanaendelea hakujatokea tishio la kuvurugwa
kwa amani wala tatizo la kiusalama. Kama hivi ndivyo, wanaFemAct
tunaendelea kuamini kuwa tamko la Vyombo vya Ulinzi na Usalama lina
agenda yake; ya siri. Si bure! Litakuwa ni jambo la kushangaza na
kusikitisha sana iwapo Watanzania watabaini kuwa vyombo vyao vya
ulinzi na usalama vimeanza kutumiwa vibaya na wanasiasa na vyama vya
siasa kwa manufaa ya kikundi maslahi binafsi cha vatu wachache.

iii). Jeshi la Wananchi wa Tanzania halipaswi kujihusisha na masuala
ya ndani ya usalama wa raia. Kama kweli kungekuwa na tishio la amani
na usalama, basi tungetegemea kuona Jeshi la Polisi, chombo chenye
dhamana ya kuhakikisha kunakuwa na hali ya usalama kwa raia na mali
zao, likitoa tamko hilo; siyo JWTZ. Sasa kama hivyo ndivyo, wanaFemAct
tunasikitika na kushangaa kuona Jeshi la Wananchi wa Tanzania
likifanya kazi za polisi wakati askari wa Jeshi la Polisi wapo tele,
pamoja na Inspekta Jenerali wao. Hali hii haieleweki na ni kinyume cha
kanuni za msingi za utawala bora. Inakuwaje askari polisi waendelee
kulipwa mshahara wakati kazi zao zinafanywa na wanajeshi wa JWTZ!

iv). Ujumbe unaotolewa na tamko la Vyombo vya Usalama kuwa
"vimejiandaa kikamilifu kupambana na mtu, watu, kikundi, chama au
taasisi yoyote... itakayochochea kuyakataa matokeo ya uchaguzi" ni
kitisho cha dhahiri, si kwa vyama vya siasa na wagombea pekee, bali
pia ni dhidi ya jitihada za kujenga na kuimarisha utawala bora na
demokrasia kwa ujumla hapa nchiniTanzania. Ni dhahiri Luteni Jenerali
Abdulhaman Shimbo anafahamu kuwa si wanajeshi wala silaha zinazoweza
kulazimisha wananchi, vyama vya siasa na wagombea wao wakubaliane na
matokeo ya uchaguzi bali uchaguzi unaokubalika miongoni mwa washindani
na wananchi kwa ujumla kuwa umefanyika kwa kuzingatia vigezo vya
msingi vya chaguzi huru na haki. Katika kutimiza hili, usimamizi imara
na usiokuwa na upendeleo, na vyombo vya usalama na vyombo vya habari
visivyopendelea upande wowote ni nguzo muhimu kuhakikisha washindani
wa kisiasa wanakubaliana na matokeo ya uchaguzi. Yaliyotokea katika
nchi za Romania, Ukraine, Zimbabwe, Kenya, Jamhuri ya Kidemokrasia ya
Kongo, Burundi na kwingineko duniani ni mifano inayotoa mafunzo ya
kutosha kwa raia na wanajeshi pia. Hakika hili halihitaji tamko la
Vyombo vya Ulinzi na Usalama. Kama hivyo ndivyo, wanaFemAct hatuoni
sababu iliyopelekea Vyombo vya Ulinzi na Usalama kutoa tamko lake, na
hasa katika kipindi hiki ambacho kampeni zinaendelea vizuri. FemAct
hatuko tayari kuona Tanzania inapitishwa ya machafuko ya kupandikiza
kwa lengo la kunufaisha kirundi maslahi cha vatu wachache.

Kwa kuzingatia sababu zetu hapo juu, wanaFemAct tunapendekeza
ifuatavyo:
a). Vyombo vya Ulinzi na Usalama viache mara moja kuingilia mchakato
wa uchaguzi kwa kuwa jambo hili linaweza kusabaisha vitisho na vurugu
dhidi ya wapiga kura na wananchi kwa ujumla; kuchafua hali ya amani na
usalama ambayo ni tunu ya Tanzania. Lakini iwapo kutakuwa na haja ya
kufanya hivyo, basi sheria husika sharti zifuatwe, Jeshi la Polisi
likiwa na dhamana ya kufanya hivyo kwa mujibu wa sheria.

b). Wanasiasa, vyama vya siasa na viongozi waache mara moja
kujitafutia ushindi kwa kutumia mlango wa nyuma. Uongozi wa dola
sharti upatikane kupitia mashindano ya wazi kusaka ridhaa ya wananchi
kidemokrasia katika uchaguzi unaokubalika kuwa huru na haki, siyo
kutumia vyombo vya Ulinzi na Usalama kutisha wapiga kura ili
kujihakikishia ushindi.

c). Vyombo vya habari viendelee kuhabarisha wananchi na wapiga kura
juu ya mipango ya sera za vyama vya siasa na ahadi za wagombea kama
inavyojiri katika mikutano ya kampeni.

d). Asasi za kiraia ziendelee kuelimisha wananchi juu masuala
mbalimbali yanayoongeza uangavu kwa wapiga kura, na wananchi kwa
ujumla juu ya sheria, taratibu, kanuni za uchaguzi, haki na wajibu wa
kuhudhuria mikutano ya kampeni, kusikiliza ahadi za wagombea, kufanya
maamuzi na hatimaye kujitokeza kupiga kura.

e). Wapiga kura waendelee kujibidisha kupata elimu ya mpiga kura,
kuhudhuria mikutano ya kampeni ya vyama vya siasa na wagombea, na
kusikiliza kwa makini ahadi za wagombea wakipembua na kuchambua kati
ya pumba na mchele ili kunako Oktoba 31 wafanye uamuzi kwa kihistoria
kuchagua viongozi watakaoweza kushirikiana na wananchi kukwamua Taifa
letu kuondokana na umaskini na kuletea Taifa heshima.


Mwisho/

FemAct

Dar es Salaam, Oktoba 6, 2010.

Kwa habari zaidi tembelea,

Tuesday, 28 September 2010

Poverty and Human Development Report 2009

Report hii nzuri sana kwa mtu anayetaka kufuatilia mambo mbalimbali ya utekelezaji wa mipango ya maendeleo na uchumi. Cheki hiyo link hapo chini usome

http://www.tz.undp.org/docs/Tanzania_PHDR_2009.pdf

The Millennium Development Goals

Assessing Progress in Africa Toward the Millennium Development Goals

MDG Report 2010

Mandated by the Assembly of Heads of State and Government of the African Union, the African Union Commission (AUC), the United Nations Economic Commission for Africa (ECA) and the African Development Bank (AfDB) have, over the past five years, jointly produced this annual re- port on Assessing Progress in Africa toward the Millennium Development Goals. This year, the three pan-African institutions have been joined in this effort by the United Nations Development Programme.

This year’s report shows that, prior to the onset of the food and fuel crises and the global recession, African countries were making steady progress toward attainment of the MDGs. Even though information is not yet available to delineate the precise impact of the three crises on MDG achieve- ment, we know that many African countries were sharply affected by these shocks. However, with support from their international development part- ners, including the African Development Bank and UNDP, African countries have taken a series of measures aimed at stemming the adverse effects.

The emerging picture of Africa in this year’s report portrays a continent that has secured progress in key areas such as net primary enrollment, gender parity in primary education, political empowerment of women, access to safe drinking water, and stemming the spread of HIV/AIDS. Antiretroviral treatment is becoming available in a large number of countries and maternal mortality rates are falling in some places. On the economic front, growth has begun to pick up after the global economic and financial crises.

The report draws attention to policy innovations in Africa that are facilitating progress toward attainment of the MDGs. These innovations include new and expanded social protection programs, which were once thought to be unaffordable to most poor countries but are now embraced as important additional interventions to secure
progress on key human development indicators. In addition, countries have used the MDGs as a framework for development planning, strengthening coordination and cascading the MDGs to lower tiers of government.

Nonetheless challenges remain, especially in the area of health. Achieving the goal of “health for all,” as embraced in Almaty about 30 years ago, has proven to be difficult. Health in Africa is still not “for all” but rather is characterized by glaring inequities among socioeconomic groups and classes. Progress in achieving the MDGs has therefore been considerably fettered by the slow progress on meeting the health targets.

The adverse impacts of climate change pose a further threat to the sustainability of MDGs achievement. Moreover mitigating climate change presents a significant policy challenge for a region that faces huge energy needs to power its development and industrialization. The continent must have access to the technology and financing that will enable it to meet those energy needs, but in a way that is consistent – to the extent possible – with climate change mitigation.
FULL REPORT IS HERE
http://www.undp.org/africa/mdg2010.shtml

MKUKUTA

Hili ndilo document la MKUKUTA.Ni bora kulisoma japo kidogo.Tembelea
http://www.tanzania.go.tz/nsgrf.html

Friday, 24 September 2010

Mauaji ya akina mama wazee

Akina mama wazee 2,585 katika mikoa 8 waliuawa kikatili katika kipindi kisichozidi miaka 5 hadi kufikia Feb 2009 kwa tuhuma kuwa ni wachawi kwa mujibu wa Kituo cha Sheria na Haki za binadamu 2009. Hao ni wale tu walioripotiwa. Hawa wazee wengine wajane wanauliwa kwa madai ni wachawi ili tu wanyanganywe mashamba na mali zingine walizoachiwa na waume zao.JE JAMANI HILI SI JANGA LA TAIFA? Wagombea wetu wanalijua hili?

Tuesday, 21 September 2010

Universal Declaration of Human Rights

Hili dude liliandikwa bwana.Linatoa mwongozo mzuri sana wa kulinda haki za binadamu na kujenga amani duniani.Ila kuna washenzi wanapenda kuharibu peace! http://www.un.org/en/documents/udhr/index.shtml

Saturday, 18 September 2010

Unamkumbuka Munga Tehenan?

Marehemu Munga Tehenan, wakati wa uhai wake alikuwa mwandishi mahiri wa habari nchini Tanzania. Baadae akaanzisha gazeti la Jitambue.Lilikuwa likitoka kila Jumatano na makala kuhusu elimu ya utambuzi. Humo ulikuwa ukipata habari za namna ya kujenga haiba yako, kujiamini na kuwa na mawazo chanya yanayoweza kusukuma mbele maisha yako na ukaishi kwa mafaniko na furaha. Munga aliandika sana akiwausia watu kubadilika na kuachana na mawazo ya kulogwa, au kuwa na nuksi katika maisha.


Jamaa hakuchoka.Alikuwa mchapa kazi akisistiza umuhimu wa kufanya kazi kwa bidii na maarifa ili kujipatia mafaniko na furaha.Alipiga vita sana mawazo hasi, akiyasema kuwa ndo chanzo cha maradhi na watu kuwa na maisha yaso na furaha wala amani.

Munga hakika nikiwa mmoja wa wasomaji wake niliipenda elimu ile ambayo aliitoa vyema akitumia mifano hai ya maisha ya hapa Tanzania.Nilipata inspiration kubwa sana baada ya kusoma habari hizo kiasi kwamba baada ya kipindi fulani nikawa mmoja wa wachangiaji katika gazeti lile.

Leo hii naweza kusema Munga alitoa mchango mkubwa sana katika kuyabadilisha maisha yangu na kuwa ya furaha. Inspiration niliyopata kutokana na juhudi zake ni kubwa mno.Hakika Yahwe amlaze mahali pema peponi amina.

Hapa chini ni moja ya makala zake kama nilivyoichukua toka blog ya ndugu Shaban Kaluse-http://kaluse.blogspot.com/2008/11/je-hayati-munga-tehenan-aliwahi.html
 


"Ili kufanikiwa kwenye lengo lolote katika maisha, ni lazima uamini kwamba utafanikiwa. Kama usipofanya hivyo, una nafasi kubwa ya kushindwa.

Unaweza kuwa na malengo mapya uliyoyapanga na ambayo unaanza kujaribu kuyatekeleza. Lakini ni lazima ufanye hivyo ukiwa na imani kubwa kwamba utafanikiwa.



Waweza kuona kazi uliyo nayo hivi sasa haikusaidii sana na hivyo kuamua ghafla kuiacha.Waweza kufanya hivyo huku ukiwa hujaamua kitu gani cha kufanya, na hivyo kulazimika kutumia kipindi cha pengine miezi sita ama hata zaidi inayofuata kujaribu kufikiria nini cha kufanya.


Huwezi kufanikiwa katika kile unachokitaka kufanya ikiwa hutaamua kuyafanya mawazo yako hayo uliyonayo kuwa vitendo. Hata ukiwa na kiu na hamu kubwa kiasi gani ya kufanikiwa, bila kuhamasisha nafsi yako na kuanza kufuatilia lile unalotaka kulifanya, kufanikiwa itakuwa ndoto kwako. Hilo litashusha ari yako na kujikuta unarudi kulekule ulikotoka, kwenye kazi ya kuajiriwa.


Lakini wakati wote huu, vyanzo vya mafanikio huwepo karibu nawe tayari kutumiwa nawe kwa ajili ya kukuletea mafanikio unayoyataka. Lakini bila kuiamini nafsi yako kwamba unaweza kufanikiwa, huwezi kufanikiwa.

Hivyo ni lazima ujifikirie katika mambo unayoyafanya, unafanya mambo yako yanayokuelekeza kwenye malengo yako ukiwa na imani kwamba utafanikiwa. Je, unayo picha ya mafanikio yako akilini mwako na hisia kwamba hivi ndivyo inavyotakiwa kuwa?

Hebu kaa chini na ufikirie kuhusu mambo uliyowahi kuyafanya na ukashindwa katika kipindi cha miaka michache iliyopita. Jiulize ikiwa kweli ulijiamini kwa dhati kwamba utafanikiwa.


Mara nyingi utakuta katika matukio hayo ulikuwa na mashaka ndani yako kuhusiana na uwezo wako wa kufanikiwa na hivyo iko haja ya kujihamasisha kabla ya kuanza kupiga hatua kuelekea kwenye lengo lako. Unatakiwa kuamini kwamba utafanikiwa.

Ni kwa nini imani hiyo ni muhimu kiasi hicho? Kwa kawaida huwa tunaanza kujenga imani tangu tukiwa wadogo. Mara baada ya kuzaliwa kwetu, huanza kujenga au kujengewa imani.

Na baadaye tunaendelea kujijengea imani wakati tukiendelea kukua na huwa tunabadili imani kutoka za zamani na kujenga mpya, kutegemea vitu vingi. Tunahitaji kufanya haya ili kuyafanya maisha yetu hapa duniani yawe rahisi na ya kweli.

Siku zote tunaamini kwamba tunapoamka vitandani mwetu asubuhi, tunahitajika kuweka miguu yetu chini ili kuweza kusimama ardhini kabla ya kuendelea na shughuli zetu nyingine na si kuruka hewani hadi kwenye dari ili kuweza kutoka vyumbani mwetu kwa shughuli zetu za kawaida.


Tumejifunza hili tangu tukiwa wadogo kabisa na sasa hatuna haja hata ya kufikiria kila siku kwamba hivyo ndivyo tunavyotakiwa kufanya. Vivyo hivyo, pia hatuna haja ya kufikiria ni kwa kiasi gani nguvu ya uvutano ina mchango gani katika kusimama kwetu kila asubuhi tangu tunapoamka vitandani mwetu.


Wakati unapofungua mlango wa nyumba yako, unageuza ufunguo wako kuelekea upande uliko ubao wa kufungia mlango ama upande wa tofauti na mwenendo wa mikono ya saa.
Hiyo ni imani tunayojijengea tangu tukiwa watoto wadogo kabisa, tunapoanza kujifunza kufungua na kufunga milango.

Kila unapokutana na mlango mpya hatuwi na wasiwasi kwamba tunajua vile mlango unavyofunguka kwani tunakuwa na hakika (akilini mwetu) na namna mlango huo utakavyofunguka. Tunazunguusha funguo kuelekea upande uliko mlango tu! Ni rahisi. Hiyo ndiyo imani tuliyonayo.


Huoni sababu ya kufikiria uwezekano wa kukutana na mlango unaofunguka vinginevyo. Lakini hakuna atakayekataa kwamba wengi tumewahi kukutana na milango inayofunguka kwa mwelekeo tofauti na ule tunaoamini ndio utaratibu ‘unaokubalika.’ Inaudhi sana unapokutana nao kwa mara ya kwanza.

Hata baada ya mwaka mzima wa kufungua mlango kwa mwelekeo huo, bado imani uliyojijengea kutokana na uzoefu wako kwamba mlango haufunguki kwa mwelekeo huo, utakuwa nayo, na hivyo utakuwa ukikasirika kila mara utakapofungua mlango huo. Imani unayojijengea moja kwa moja huathiri tabia yako, hata kama imani hiyo si sahihi kama unavyofikiria.


Hebu tufikirie kitu kingine! Dunia ni duara ama si duara? Umelijuaje hili? Si kwamba umeambiwa na watu tu? Una uhakika gani? Wapo wanaoamini kwamba dunia ni ya ubapa kutokana na wanavyoiona kila wanapochungulia madirishani.


Kama ungeamini kwamba dunia ni ya ubapa, ni wazi ungepatwa na wasiwasi mkubwa wakati unaposafiri kwenye mashua kwamba huenda mngefika mwisho na kuangukia nje ya dunia.

Lakini hivi ndivyo watu walivyokuwa wakifikiria. Kilikuwa ni kikwazo kikubwa kwa ugunduzi kwa miaka mingi ya mwanzoni. Imani waliyokuwa nayo watu moja kwa moja iliathiri vitendo vyao, na hilo lilikwaza matokeo yao.


Fahamu tena kwamba imani si lazima zioneshe ukweli uliopo duniani. Si kila siku milango hufunguliwa kuelekea mwelekeo uliko mlango.


Imani kuhusu dunia kuwa ubapa ilibadilishwa mara wagunduzi walipoanza kuzunguuka dunia. Imani huathiri moja kwa moja matendo yetu hata hivyo. Wakati mwingine, tunachukua hatua hata imani zetu zinapokuwa si sahihi, na hii yaweza kutukwaza. Hii ni kweli kuhusiana na imani tulizonazo kuhusu nafsi zetu na uwezo wetu.

Vipi kuhusu nafsi zetu? Kama tufanyavyo mambo tuliyoyazoea bila kufikiria kutokana na imani tunazojijengea kama vile kufungua mlango, tunafanya hivyo hivyo kutokana na imani tunazojijengea kuhusu nafsi zetu.
Ikiwa tutajenga imani za kutukwaza kuhusiana na nini kinawezekana kufanikisha, jibu letu litakuwa kukwamisha matokeo ya vitendo vyetu tunavyochukua. Matokeo yake tunakwaza pia matokeo tunayoyapata.


Ikiwa tunaamini kwamba kuna kila uwezekano wa kushindwa katika kile tunachofanya mawazo yetu ya kina (subconscious mind), itafanya kazi ya kujenga mazingira yatakayounga mkono imani yetu hii. Wakati mambo yanapokuwa magumu, hatutakuwa na haja ya kufanya jitihada zaidi iliyo muhimu katika kufanikiwa; kushindwa kwa mara ya kwanza kutaunga mkono imani yetu hiyo na hivyo kutufanya tukate tamaa na kuachana na kile tunachofanya.


Kwa upande mwingine, ikiwa tutaamini kwamba tutafaulu, ni lazima tutafaulu. Mohamed Ali aliyekuwa akifahamika kama mwanamichezo aliyefanikiwa kushinda wote waliowahi kutokea duniani, mbali ya ari aliyokuwa nayo, kipaji na nguvu zake, moja ya sababu kuu zilizomsadia kufanikiwa na kuwa maarufu kiasi alichokuwa ni kwamba alikuwa na imani nzito kuhusiana na kila alichotaka kufanya.


Wengi tumewahi kuona picha zake za televisheni wakati akiwa ulingoni, alipokuwa akidai kwamba yeye ndiye bondia bora kushinda wote waliowahi kutokea duniani. Wakati alipokuwa akiieleza dunia hivi, ni kweli alikuwa bondia bora kushinda wote duniani? Wakati ule hakuwa hivyo, kwani alikuwa bado ana mambo ya kuionesha dunia ili kuthibitisha hilo. Alichokuwa nacho hata hivyo ni kujiamini moja kwa moja katika uwezo wake. Imani hiyo ilithibitishwa na matokeo aliyoyapata licha ya kuvuliwa mkanda wake wa dunia mwaka 1967, baada ya kukataa kwenda kupigana vita Vietnam akiwa askari wa jeshi la Marekani, hakukata tamaa.


Alirudi tena miaka saba baadaye na kushinda ubingwa huo alioendelea kukaa nao kwa miaka minne zaidi. Imani yake kwamba yeye ndiye bora kuliko wote waliowahi kutokea duniani, si kwamba ilimsaidia kufikia kiwango cha juu cha masumbwi, bali kiwango cha juu cha michezo kwa ujumla



Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wengi wetu sijui kama tumewahi kuisoma katiba ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania. Cheki link na usome sasa.http://www.tanzania.go.tz/images/katibamuungano.pdf